Swahili
سورة Al-Humazah ( The Slanderer ) - عدد الآيات 9
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
Hakika huo utafungiwa nao
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.