Swahili

Surah As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya count 182
Share
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.