Swahili

Surah Al-Mu'minoon ( The Believers ) - Aya count 118
Share
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa sababu wananikanusha.
(Mwenyezi Mungu) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta.
Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia.
Na huku mkitakabari na usiku mkiizungumza (Qur'ani) kwa dharau.
Na lau tungeli warehemu na tukawaondolea shida waliyo nayo bila ya shaka wangeli endelea katika upotofu wao vile vile, wakitangatanga.
Watasema: (Ufalme huo) ni wa Mwenyezi Mungu. Sema: Basi vipi mnadanganyika?